Friday, September 29

Biashara

Rais Dk. Mwinyi azungumza na  wafanyabiashara na wadau  wake  kujadili mustakbali wa bei za bidhaa hasa vyakula.  
Biashara

Rais Dk. Mwinyi azungumza na wafanyabiashara na wadau wake  kujadili mustakbali wa bei za bidhaa hasa vyakula.  

    SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanya juhudi za makusudi kudhibiti mfumko wa bei hasa kwa bidhaa za chakula nchini. Aidha, imetoa agizo kwa wafanyabiashara wote wa vyakula kupunguza bei ya sukari ambayo ushuru wake kwa Zanzibar ni mdogo zaidi kuliko popote duniani. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na wafanyabiashara mbalimbali nchini, wazalishaji wanaoingiza bidhaa na mizigo na wadau wote wa biashara zikiwemo taasisi za Serikali na binafsi kujadili mustakbali wa bei za bidhaa hasa vyakula  zinazopanda kila uchao. Rais Dk. Mwinyi aliwaeleza wanafanyabiashara hao kuwa karibu na kuzungumza na Serikali wakati wote kunapotokea matatizo badala ya kuwapandishia bei wanan...
Tigo Zantel yatoa zawadi kwa wakulima wa karafuu Pemba
Biashara

Tigo Zantel yatoa zawadi kwa wakulima wa karafuu Pemba

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA   MDHAMINI wa shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Pemba Abdalla Ali Ussi, amewashauri wakulima wa zao la karafuu Kisiwani humo, kuendelea kupokea fedha zao za mauzo ya karafuu kwa kutumia mtandao wa TigoPesa.   Alisema asilimia 85 ya wakulima kisiwani hapa, bado wanapokelea fedha zao mkononi, jambo ambalo linasababisha upotevu wa fedha kwa shirika na baadhi ya wateja kuibiwa fedha zao.   Mdhamini huyo aliyaeleza hayo katika hafla ya kuwakabidhi zawadi kwa wakulima bora wa karafuu, ambao wametumia huduma ya TigoPesa wakati wakupokea malipo yao kwa kipindi cha mwezi wa Agosti 2023.   Alisema ZSTC inatumia njia tatu za kulipa fedha kwa wakulima baada ya kuuza karafuu zao katika shirika hilo, moja Bank, TigoP...
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla azungumza na wadau wa Bandari.
Biashara

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla azungumza na wadau wa Bandari.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imemkabidhi muwekezaji kusimamia huduma za uendeshaji wa Bandari ya Zanzibar ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa wafanayabishara na wananchi. Ameyasema hayo alipokutana na wadau wa Bandari wakiwemo Mawakala wa ushushaji na upakiaji wa mizigo, wamiliki wa meli na wamiliki wa majahazi pamoja na wafanyabiashara katika kutathmini utendaji na uendeshaji wa shughuli za bandari. Mhe. Hemed amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussen Ali Mwinyi ina dhamira njema ya kuleta mabadiliko ya kiutendaji katika Sekta ya Bandari kwa lengo la kuleta ufanisi wa huduma za bandari. Amefahamisha kuwa lengo la kupewa Muwekezaji kuiendesha Bandari ya Zan...
NMB YADHAMIRIA KUFUNGUA TAWI WETE
Biashara

NMB YADHAMIRIA KUFUNGUA TAWI WETE

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amelitaka jeshi la Polisi Mkoa huo kuzitumia ipasavyo Kompyuta walizokabidhiwa kwa kuhifadhi taarifa zao kisasa, ili kuwatia moyo wadau waliowasaidia kwa kuwapatia Vifaa vyengine. Alisema ili kuwatia moyo NMB ni kuvitumia kwa lengo lililokusudiwa, pamoja na kuvitaunza vikadumu kwa muda mrefu, kwa saivi jeshi hilo linapaswa kwenda kisasa zaidi. Mkuu huyo aliyaeleza hayo katika hafla ya kupokea na kukabidhi kompyuta mbili zilizotolewa na benk ya NMB kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini, hafla iliyofanyika makamo makuu wa jeshi hilo Wete. Alisema Bank ya NMB imekua ikiunga mkono juhudi mbali mbali zinazoanzishwa na Serikali za SMZ na SMT, hususan juu ya matumizi ya mfumo wa Tehama katika utenda...
Biashara, Sheria

Wadau wa Sheria wajadili na  kutoa Maoni  katika  rasimu ya sheria ya kuanzishwa mahakama maalum  ya rushwa  na uhujumu uchumi.

NA AMINA AHMED-PEMBA. WADAU wa sheria kutoka Taassisi mbali mbali za Serikali pamoja na taasisi binafsi  kisiwani Pemba  wameshiriki katika  mkutano maalumu wa kujadili na  kutoa Maoni  katika  rasimu ya sheria ya kuanzishwa mahakama maalum  ya rushwa  na uhujumu uchumi   uliondaliwa na  ofisi ya mwanasheria mkuu Zanzibar   wenye lengo la kuboresha na  kupatikana kwa sheria  bora  itakayosimamia masuala hayo.   Wakitoa maoni yao mara baada ya kufanyiwa mapitio ya rasimu hiyo  baadhi ya wadau hao  akiwemo Muhammed  Ali  Muhammed   kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka,  Simba Khamis Simba  kutoka  kikosi cha kuzuia magendo Zanzibar   (KMKM)  wameiomba kamati  inayosimamia   rasimu hiyo kuongeza Vifungu vya sheria  ambavyo vitaweza kusimamia suala la usafirishaji haram wa mage...