Rais Dk. Mwinyi azungumza na wafanyabiashara na wadau wake kujadili mustakbali wa bei za bidhaa hasa vyakula.
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanya juhudi za makusudi kudhibiti mfumko wa bei hasa kwa bidhaa za chakula nchini.
Aidha, imetoa agizo kwa wafanyabiashara wote wa vyakula kupunguza bei ya sukari ambayo ushuru wake kwa Zanzibar ni mdogo zaidi kuliko popote duniani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na wafanyabiashara mbalimbali nchini, wazalishaji wanaoingiza bidhaa na mizigo na wadau wote wa biashara zikiwemo taasisi za Serikali na binafsi kujadili mustakbali wa bei za bidhaa hasa vyakula zinazopanda kila uchao.
Rais Dk. Mwinyi aliwaeleza wanafanyabiashara hao kuwa karibu na kuzungumza na Serikali wakati wote kunapotokea matatizo badala ya kuwapandishia bei wanan...