Sunday, March 26

ELIMU

Watoto watoro warudishwa skuli
ELIMU

Watoto watoro warudishwa skuli

NA ABDI SULEIMAN. KAMATI ya Kupambana na Vitendo vya Udhalilishaji shehia ya Ndagoni, imeweza kuwarudisha skuli watoto 40 na kujiunga na darasa mbadala, huku 15 kayi yao hawakuwahi kusoma hata darasa la kwanza. Kamati hiyo imesema watoto 25 waliweza kuacha skuli kutokana na sababu mbali mbali, waliobakia wakianza sasa kusoma baada ya kukosa elimu hapo awali. Mwandishi wa habari hizi alishuhudia baadhi ya wanafunzi wakiendelea na masomo yao katika skuli hiyo, huku wengi wao wakionekana ni wale waliokatisha kuendelea na masomo huko nyuma. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mratib wa wanawake na watoto shehia ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake, Shuwarika Ali Mohamed, alisema kamati hiyo imeundwa kufuatia kupatiwa elimu na Taasisi ya KUKHAWA Pemba, chini ya mradi wa kata...
Kamati ya skuli ya sekondari furaha yatakiwa kushirikiana na walimu  kuondosha  changamoto ya utoro wa wanafunzi katika skuli hiyo.
ELIMU

Kamati ya skuli ya sekondari furaha yatakiwa kushirikiana na walimu kuondosha changamoto ya utoro wa wanafunzi katika skuli hiyo.

NA HANIFA SALIM, PEMBA. MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud ameitaka kamati ya skuli ya sekondari furaha kushirikiana na walimu ili kuhakikisha wanaondosha changamoto ya utoro wa wanafunzi katika skuli hiyo. Alisema, kuna baadhi ya wazazi wanadhani jukumu la kumsimamia mtoto kusoma ni la walimu pekee jambo ambalo linasababisha kwa kiasi kikubwa utoro pamoja na matokeo mabaya katika mitihani yao ya taifa. Akizungumza kwa niaba Mkuu wa Mkoa huyo Katibu Tawala Mkoa wa Kusini Pemba Suleiman Hamad aliyasema hayo, katika sherehe ya mahafali na kuwakabidhi zawadi wanafunzi waliofaulu vizuri kidato cha nne, darasa la saba na la nne iliyofanyika skuli ya Furaha Chake chake. "Wanafunzi 11 ambao wamefaulu si kidogo lakini pia sio wengi, ni imani yangu mwaka huu 2023 i...
KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR AWAAGIZA TRAFFIC KUSIMAMIA USALAMA WA WATOTO BARABARANI
ELIMU, Kitaifa

KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR AWAAGIZA TRAFFIC KUSIMAMIA USALAMA WA WATOTO BARABARANI

NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad amewaagiza Askari wa Kikosi cha Usalama barabarani kuongeza ulinzi wa watoto wakati wanapokwenda na kurudi shule ili kuepusha ajali zinazosababisha vifo na majeruhi kwa watoto. Akisikiliza kero za wananchi wa Shehia za Fuoni Uwandani, Migombani, Kipungani, Kibondeni, Chunga na Mambosasa Wilaya ya Magharibi B huko Skuli ya Fuoni amesema elimu inahitajika kwa Askari, madereva, abiria na watumiaji wengine wa barabara juu ya matumizi sahihi ya barabara na alama za usalama barabarani. (more…)
TAMWA-ZNZ yaanza mkakati mpya  kushuka mashuleni kutoa elimu ya udhalilishaji
ELIMU, Kitaifa, Wanawake & Watoto

TAMWA-ZNZ yaanza mkakati mpya kushuka mashuleni kutoa elimu ya udhalilishaji

Zaidi ya wanafunzi 300 kutoka shule mbili za wilaya ya mjini Unguja leo wamepatiwa mafunzo ya kujikinga na kutambua viashiria vya udhalilishaji katika maisha yao ya kila siku. Shule hilzo ni Memon ya Stown Town na Bubu ambapo maafisa wa TAMWA-ZNZ kwa kushirikiana na mitandao ya kupinga udhalilishaji (GBV network) wamekuna na kutoa elimu kwa wanafunzi hao kwa nyakati tofauti. Wakati wakitoa elimu maafisa hao  wakiongozwa na afisa anashughulikia maswala ya udhalilishaji TAMWA-ZNZ Zaina  Salum amesema wameamua kuwafikia wanafunzi mashuleni kutokana na sababu mbali mbali. Alisema kwa kipindi kirefu wamekua wakitoa elimu kupitia vyombo vya habari jambo ambalo wanadhani kuna wakati elimu hiyo haifiki kwa walio wengi na ndio maana kila leo matendo hayo yamekua yakifanyika. "Unajua...
Bado vijana wadai kuzongwa na umaya umaya wa changamoto
Biashara, ELIMU, Kitaifa, Makala, vijana

Bado vijana wadai kuzongwa na umaya umaya wa changamoto

PAMOJA NA JUHUDI ZA SERIKALI KWA VIJANA Bado vijana wadai kuzongwa na umaya umaya wa changamoto   NA ABDI SULEIMAN, PEMBA SOTE tunafahamu kuwa vijana ndio tegemeo kubwa la taifa na ndio wazalishaji wakubwa katika nchi yoyote ile ulimwenguni. Miongoni mwa mazingira hayo kuanzishwa kwa baraza la Vijana, uwepo wa sera ya vijana, kuwepo na mikakati mbali mbali inayosimamia vijana, asasi mbali mbali za kiraia nazo zimekua na mchango mkubwa katika kusaidia vijana. VIJANA WENYEWE WANASEMAJE Maryam Mussa Salum (22) mkaazi wa Ng’ambwa, anasema changamoto kubwa ni kuwezeshwa, upatikanaji wa mitaji na elimu ya kutoka, kwani bila ya elimu hakuna linaloweza kufanyika. “Mfano kijana anakwambia ndoto yake ni kufanya biashara, lakini hana elimu wala mtaji, unadhani anaweza kufikia...