Sunday, March 26

Michezo

KIKUNDI cha mazoezi cha Mtu ni Afya Fitness Club cha Kidike  kutembea shehia hadi shehia, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi
Michezo

KIKUNDI cha mazoezi cha Mtu ni Afya Fitness Club cha Kidike kutembea shehia hadi shehia, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi

KIKUNDI cha mazoezi cha Mtu ni Afya Fitness Club cha Kidike, kimesema kinakusidia kutembea shehia hadi shehia, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kufanya mazoezi, ili kuwatayarisha vijana kushiriki katika michezo mbali mbali. Kauli hiyo imetolewa na mbunge wa jimbo la Kojani Hamad Hassan Chande, baada ya kumaliza matembezi yalioanzia Mchangamdogo hadi Madenjani na ufanyaji wa mazoezi ya Viungo, pamoja na kukabidhi Jezi na Fedha taslimu kwa ajili ya bonanza la michezo linalotarajiwa kufanyika Januari Mosi 2021.   Alisema kupitia vikundi hivyo anaamini kwamba upo uwezekano mkubwa wa kuibua vipaji mbali mbali vya michezo, ikiwemo mchezo Riadha, mpira wa miguu na resi za baskeli, ambapo watakua na uwezo wa kushiriki michezo mbali mbali ya kitaifa na kimataifa. Aliwa...
DK.Mwinyi asikitishwa na viongozi wa vyama vya michezo
Michezo

DK.Mwinyi asikitishwa na viongozi wa vyama vya michezo

    RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi, amewataka viongozi wa vyama vya michezo Zanzibar kusimamia michezo kwa uweledi ili kurudisha hadhi ya michezo ambayo imepotea Zanzibar. Dkt. Mwinyi alisema tayari alishamuagiza waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar, kukaa na wadau wa michezo na ili kuondosha tafauti zao kwa lengo la kuendeleza michezo nchini. Kauli hiyo aliitoka katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari Fidel Castro, wakati alipokua akizungumza na makundi mbali mbali ya wajasiriamali wakiwemo wanamichezo, ikiwa ni ziara yake ya siku mbili Kisiwani Pemba. Alisema lazima uongozi wa vyama vya michezo ujipange, kwani paemba walifika hadi kutaka ligi ichezwe kwao na Unguja kwao, baadae timu zikutane na kutafu...
Vilabu 16 kutoka katika jimbo la Wawi vyalipiwa ada ya usajili wa mashindano.
Michezo

Vilabu 16 kutoka katika jimbo la Wawi vyalipiwa ada ya usajili wa mashindano.

JUMLA ya Vilabu 16 kutoka katika jimbo la Wawi, vinavyoshiriki ligi za madaraja mbali mbali Kisiwani Pemba, vimekabidhiwa fedha taslimu kwa ajili ya kulipia ada ya usajili wa mashindano, katika madaraja wanayoshiriki kutoka kwa Mbunge na Mwakilishi wa jimbo hilo. Vilabu vilivyokabidhiwa fedha hizo ni daraja la kwanza walipata shilingi laki nne, daraja la Pili Mkoa walipewa laki tatu na nusu na daraja la Pili Wilaya walipatiwa shilingi laki mbili, fedha hizo ikiwa ni ahadi zilizotolewa na mbunge na mwakilishi wa jimbo hilo. Akizungumza na viongozi wa Vilabu aliyekuwa Mdhamini wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba, Fatma Hamad Rajab aliwapongeza viongozi hao wa jimbo la wawi, kwa kuwasaidia fedha za usajili vilabu ikiwa ni utekelezaji wa ahadi walizozitoa wakati waki...
MBUNGE wa Jimbo la Kojani amekabidhi vifaa mbali mbali vya michezo kwa vilabu 19.
Michezo

MBUNGE wa Jimbo la Kojani amekabidhi vifaa mbali mbali vya michezo kwa vilabu 19.

  MBUNGE wa Jimbo la Kojani Wilaya ya Wete Hamad Hassan Chande, amekabidhi vifaa mbali mbali vya michezo kwa vilabu 19 vinavyoshiriki ligi madaraja mbali mbali Kisiwani Pemba. Msaada huo uliotolewa ni seti zajezi na mipira kwa timu hizo 19 za kwanza zilizomo ndani ya jimbo hilo, huku timu zilizobakia zikitarajiwa kupatiwa wiki ijayo. Akikamibidhi msaada huo Mbunge Huyo wa Jimbo la Kojani, alisema lengo ni kuhakikisha anainua viwango vya michezo kwa vijana wa waliomo ndani ya jimbo hilo pamoja na majimbo ya jirani. Alisema kwa sasa amebakiwa na madeni mawili katika sekta ya michezo, kwa kubakia viwanja vitatu ambavyo hajavitengeneza na tayari vitatu alishavitengeneza kwa awamu ya kwanza. Alisema deni la pili ni timu mbili kuwakabidhi posi za magoli, kwa ajili ya ...
Mahafali ya 10 ya skuli ya maandalizi Star  yafana.
Michezo

Mahafali ya 10 ya skuli ya maandalizi Star yafana.

  MKURUGENZI wa Elimu ya Msingi na Maandalizi kutoka Baraza la Mji Chake Chake Makame Pandu Khamis, amewataka wazazi au walezi kuhakikisha wanaitekeleza kwa vitendo mikaba wanayopewa skuli, wakati wanapokwenda kuwaandikisha watoto wao ili kuepuka migogoro inayotokea baadae. Alisema kumekua na tabia ya wazazi kutokuifuata kimilifu mikataba hiyo, baada ya watoto wao kukubaliwa katika skuli walizowapeleka. Mkurugenzi huyo aliyaeleza hayo wakati wa mahafali ya 10 ya skuli ya maandalizi Star Nursery school iliyopo kichungwa Wilaya ya Chake Chake, pamoja na kuzungumza wazazi na walezi wa watoto. Alisema iwapo wazazi watashindwa kutekeleza kwa vitendo mikataba wanayopewa skuli, skuli hizo zitakosa maendeleo ikizingatiwa hazina bajeti wala ruzuku kutoka serikalini. “Niv...