Sunday, March 26

Wanawake & Watoto

UNESCO, TAMWA-ZNZ yasaini makubaliano kupambana na udhalilishaji ZNZ.
ELIMU, Kitaifa, Wanawake & Watoto

UNESCO, TAMWA-ZNZ yasaini makubaliano kupambana na udhalilishaji ZNZ.

Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA-Zanazibar) zimesaini mkataba wa mradi  kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuandika habari za kukabiliana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Mradi huo wa miezi mitatu wenye thamani ya dola za Marekani 17,000, umesainiwa kati ya Mkurugenzi wa TAMWA Zanzibar, Dk. Mzuri Issa Ali na Mwakilishi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Michael Toto, katika hafla iliyofanyika Tunguu Wilaya ya kati Unguja. Akizungumza katika hafla hiyo, Dk. Mzuri alisema mradi huo  utaongeza nguvu mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto ambayo ni moja ya mikakati inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Rais, Dk. H...
Watoto walindwe dhidi ya vitendo vya udhalilishaji
Wanawake & Watoto

Watoto walindwe dhidi ya vitendo vya udhalilishaji

  Wadau wa haki za watoto hasa watoto wenye umri wa zaidi ya miaka 10  wanahitaji kujadili na kuweka mpango mzuri wa kuwalinda dhidi ya  vitendo vya udhalilishaji na ukatili. Taakwimu zilizotolewa hivi karibuni na Afisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinaonesha kuwa   jumla ya watoto 1, 173 waliathirika  na vitendo vya udhalilishaji na ukatili mwaka 2022. Kwa mujibu wa taarifa hiyo jumla ya matukio 883 (asilimia 75%) ambayo yaliripotiwa ni kwa watoto hao wenye umri kati ya miaka 11 hadi 17. Kwa mukhtadha huo, TAMWA-ZNZ inaona kuna umuhimu mkubwa wa kulipa kipaumbele kundi hili na kuona ni matatizo gani yanayolikabili ili kutafuta muafaka wa tatizo. Utafiti wa kihabari wa TAMWA ZNZ uligundua kuwa matatizo ya matumizi mabaya ya kimtandao kwa vijana wa kiume ...
FAMILIA ZENYE WATOTO WENYE ULEMAVU PEMBA WAKUMBUSHWA JAMBO
ELIMU, Wanawake & Watoto

FAMILIA ZENYE WATOTO WENYE ULEMAVU PEMBA WAKUMBUSHWA JAMBO

NA HAJI NASSOR, PEMBA. WAZAZI na walezi kisiwani Pemba, wamekumbushwa kuwa, sio haki watoto wenye ulemavu kukoseshwa haki zao za msingi, kama elimu na kuchanganyika na wenzao, kwa sababu ya ulemavu walionao. Hayo yameelezwa na Mratibu wa Idara ya watu wenye ulemavu kisiwani humo, Mashavu Juma Mabrouk, wakati akizungumza na wazazi, walezi na wanafunzi wa madrssa za Umi ya Vikunguni na ile ya Annajah ya Machomane Chake chake, kwenye ziara iliyoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar. Alisema, bado baadhi ya wazazi na walezi, wamekuwa wakijenga dhana kuwa, mtoto mwenye ulemavu anahiari ya kumpatia elimu, na asiyekuwa na ulemavu ndio mwenye haki kamili. Alieleza kuwa, dhana hiyo isiwapitikie wazazi hata siku moja katika maisha yao, na badala yake wawe na haki sawa...
ELIMU, Wanawake & Watoto

Viongozi wa Dini Kuwaelimisha zaidi Wananchi hasa wa Vijijini juu ya Malezi ya Watoto kwa Kuzingatia Misingi ya Dini Zao

Na.Maulid Yussuf - Pemba. Afisa Mdhamin Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bw.Hafidh Ameir Shoka, amewataka viongozi wa dini kuwaelimisha zaidi wananchi hasa wa vijijini juu ya malezi ya watoto kwa kuzingatia misingi ya dini zao ili kusaidia kupunguza vitendo vya udhalilishaji kwa watoto. Amesema hayo wakati akifungua mkutano wa viongozi wa dini juu ya uwasilishaji wa utekelezaji wa kazi zao za kipindi cha Oktoba hadi Disemba pamoja na mikakati yao ya kipindi cha Januari hadi machi, katika Ukumbi wa Samail Hoteli Gombani Pemba. Amesema ni jambo linalotia aibu kwa Zanzibar ambayo watu wake asilimia kubwa wapo katika misingi ya kidini lakini vitendo vya  udhalilishaji kila kukicha vimekuwa vikiripotiwa. Amesema ni lazima kuongeza nguvu kwenye  mapambano hayo kwa ku...
ASASI ZA KIRAIA ZATAKIWA KUJIKITA ZAIDI KUELIMISHA ATHARI ZA UKATILI  NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA.
Kitaifa, Wanawake & Watoto

ASASI ZA KIRAIA ZATAKIWA KUJIKITA ZAIDI KUELIMISHA ATHARI ZA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA.

  Na shaib kifaya Pemba. Afisa MdhaminiWizara ya afya Kisiwani Pemba Dr. khamis Bilali Ali, amewataka wanaharakati wa asasi za kiraia wa kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kuendelea kuelimisha Jamii katika kujikinga na kujiepusha na madhara ya matendo hayo. Kauli hiyo ametoa hako ukumbi wa Samail Gomban Chake chake kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Chake Abdalla Rashid Ali, katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga  ukatili na udhalilishaji dhidi ya Wanawake na watoto. Alisema chimbuko la maadhimisho hayo linatokana na tamko La katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Kofi Annan  la mwaka 2006 kwa mataifa yote kujua ukubwa wa tatizo la ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto wakike. Afisa Mdhamini huyo alisema vitendo vya udhalilishaji bado nit...