Sunday, March 26

Wanawake & Watoto

Tuhuma za kutorosha na kubaka bado zamsotesha rumande.
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Tuhuma za kutorosha na kubaka bado zamsotesha rumande.

  Mtuhumiwa Bakar Mbwana Juma mwenye umri wa miaka 32 mkaazi wa Jomvu Kengeja anaekabiliwa na shitaka la Kumtorosha na Kumbaka msichana mwenye umri wa 17 ameiambia mahakama ya Mkoa Chake Chake kuwa yeye hahusiki na tukio hilo kwani muda uliotajwa kutenda kosa hilo alikua kwenye kibanda akinywa kahawa. Aliambia mahakama hiyo kuwa yeye ni mfanya kazi wa ujenzi wa nyumba hivyo anakawaida ya kurudi kazini  baina ya saa moja hadi saa moja na nusu za usiku na mara zote hufikia kwenye mkahawa kabla ya kwenda anakoishi. Alidai kuwa siku ambayo alituhumiwa kufanya tukio hilo alirudi kazini majira ya moja za usiku na kifikia mgahawani na kupata kahawa akiwa yeye na marafiki zake. Alifahamisha kuwa baada ya kunywa kahawa alirudi nyumbani na kuigia chooni kwa ajili kujiandaa na sa...
Umasikini ni chanzo za udhalilishaji.
Kitaifa, Siasa, Wanawake & Watoto

Umasikini ni chanzo za udhalilishaji.

UMASKINI uliokithiri  imebainika kuwa  ni moja ya  sababu inayopelekea  Watoto   kufanyiwa  Udhalilishaji. Hayo yamesemwa na wdau wa mtandao wa kupinga udhalilishaji kutoka Wilaya ya Mkoani, katika mkutano wa uwasilishaji wa ripoti za utekelezaji wa majukumu yao ya kutoa elimu  juu ya madhara ya udhalilishaji wa kijinsia kwa jamii uliofanyika ofisi ya TAMWA Pemba. Kwa upande wake Shaban Juma Kassim Msaidizi wa sheria kutoka  shehia ya Mkanyageni, alifahamisha  kuwa udhalilishaji unafanyika zaid kwa watoto  wanaokosa  malezi  ya  pamoja  ambao wazazi wao wameachana. Alisema  takriban  watoto  wengi ambao wazazi wao wameachana, wanakosa masomo na badayake wanatumikishwa ili wapate mahitaji yao  hali ambayo inaridisha nyuma maendele ya watoto. ‘’Wanawake wengi hususan wanaois...
Rushwa muhali bado ni tatizo kukomesha vitendo vya udhalilishaji.
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Rushwa muhali bado ni tatizo kukomesha vitendo vya udhalilishaji.

Licha ya juhudi mbali mbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na Asasi za kiraia kuielimisha Jamii madhara ya Udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto  na jinsi ya kutoa ushahidi kwa kesi hizo lakini bado inaonekana matendo hayo  yanaendelea kujitokeza  kutokana na Muhali uliopo kwa Wanajamii. Hayo yamesema na wajumbe wa Mtandao wa  kupinga Udhalilishaji kutoka Wilaya ya Mkoani  katika kikao  cha uwasilishaji wa ripoti za utekelezaji wa majukumu yao ya kutoa Elimu  juu ya madhara ya Udhalilishaji wa Kijinsia kwa Jamii huko ukumbi wa Chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar  [ Tamwma]  Mkanjuni Chake chake Pemba. Wanajamii hao. Wamesema Jamii inaonekana kuyafumbia macho na kuyafanyia suluhu Mitaani matendo ya udhalilishaji jambo ambalo linasababisha kuongezeka sikuhadi...
Dk. Hussein Ali Mwinyi:  kama nikipata ridhaa ya kuwa rais wa Zanzibar, nitahakikisha kunatungwa sheria, ambayo itawawezesha wajane kupata haki zao stahili.
Biashara, Kitaifa, Sheria, Siasa, Wanawake & Watoto

Dk. Hussein Ali Mwinyi: kama nikipata ridhaa ya kuwa rais wa Zanzibar, nitahakikisha kunatungwa sheria, ambayo itawawezesha wajane kupata haki zao stahili.

NA MWANDISHI WETU, PEMBA .   MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kama akipata ridhaa ya kuwa rais wa Zanzibar, atahakikisha kunatungwa sheria, ambayo itawawezesha wajane kupata haki zao stahili, kama yalivyo makundi mengine. Alisema anaelewa changamoto kadhaa zinazowakumba wanawake hao, iwe kwa wale wanaoachwa au kufiwa na waume, kwa kukoseshwa haki zao na kutupiwa mzigo wa malezi na huduma kwa watoto. Mgombea huyo wa urais, aliyasema hayo ukumbi wa zamani wa baraza la Wawakilishi mjini Wete Pemba, alipokuza akizungumza na wanachama wa jumuiya ya wajane Zanzibar kwa upande wa Pemba. Alisema, anatambua kuwa Zanzibar lipo kundi kubwa la wajane ambalo linaendelea kuteseka na kuhangaika huku na kule na wale wanaume w...