Monday, May 20

Makala

PPC kuvitangaza vivutio vya Utalii kISIWANI Pemba , Kuunga mkono kauli ya Rais wakiwa kama waandishi   ni wajibu wao.
Makala

PPC kuvitangaza vivutio vya Utalii kISIWANI Pemba , Kuunga mkono kauli ya Rais wakiwa kama waandishi   ni wajibu wao.

Na Maryam Talib – Pemba. HAKIKA kuweza nikujiwezesha hakuna kitu kinachokuja bila ya kujishuhulisha hayo ni maneno ya bwana  Hamad Salim mwenye umri wa miaka (65) alipoamua kuanzisha shamba lake la viungo lililopo sehemu moja inayopatikana Gando katika shehia ya Gando mkoa wa  kaskazini Pemba. Kilimo cha viungo ni fursa adhimu iliyopuuzwa na kufichika katika  Kisiwa cha Pemba ambayo kama ingetumiwa vyema na wakaazi wa kisiwa hichi ingekuwa na manufaa makubwa hasa hasa kwa  utalii wa ndani  na kwa wananchi wa kawaida . Hata hivyo kuna fursa moja muhimu iliyofichika kwa wakaazi wa kisiwa cha Pemba ambayo takribani miaka saba sasa anaitumia Bwana Hamad Salim wa Gando nayo ni ya kilimo cha viungo ikiwamo kilimo cha vanilla, hiliki, midalasini, tangawizi, majano, pilipili manga na ...
ZAINA FOUNDATION MKOMBOZI WA WANAWAKE KATIKA KUTUMIA DIGITALI TANZANIA.
Makala

ZAINA FOUNDATION MKOMBOZI WA WANAWAKE KATIKA KUTUMIA DIGITALI TANZANIA.

  NA, AMINA AHMED MOH’D-PEMBA.  ZAITUNI Abdulkarim Njovu ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Zaina Foundation inayotetea haki  ya kutumia mitandao ya kijamii kwa wanawake Tanzania.  Taasisi hiyo ambayo makao makuu yake makuu yake ni Dar es Salam  ilianza harakati hizo  mwaka 2017  na kufika Zanzibar  mwaka 2022. Zaituni alisema walifikia uamzi wa kuwa na hio taasisi baada ya kugundua kuwepo changamoto nyingi, ikiwemo ya ukatili wa kijinsia mtandaoni. Vile vile zipo changamoto za kiuchumi, kiwango cha chini cha elimu ya matumizi sahihi ya mtandao na wanawake kidogo kutumia haki hiyo . Vile vile sheria sio rafiki kwa mwanamke kukingwa anapofanyiwa udhalilishaji mtadaoni. Kwa mujibu wa takwimu  za sensa ya watu na makazi za  mwaka 2022 Tanzan...
Zawadi: Mwakilishi wa Konde anaepambania kuzitatua changamoto za wananchi.
Makala

Zawadi: Mwakilishi wa Konde anaepambania kuzitatua changamoto za wananchi.

‘Asema, watu wayasemee mazuri anayoyatekeleza sio kumbeza’ NA ZUHURA JUMA, PEMBA "NIMECHIMBA visima nane katika Jimbo langu, visima sita ni vipya na viwili vilikuwepo zamani lakini vilikuwa havitumiki tena kutokana na uchakavu," si maneno ya mtu mwengine bali ni ya mwakilishi wa Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor. Zawadi ni mwanamke anaepambania kuzimaliza changamoto ndani ya jimbo lake ambazo zilikuwa zikimkosesha usingizi kabla ya kuwa kiongozi. Mama huo wa makamo anaendelea kutimiza malengo yake aliyojiwekea baada ya kuingia kwenye chombo cha kutoa maamuzi, ambayo ni ndoto yake ya muda mrefu. Katika kipindi hiki cha muda mfupi cha uongozi wake, amefanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa visima, hali ambayo imewapunguzia usumbufu wananchi hasa wanawake na wa...
MAKALA: Ukosekanaji wa fidia  kwa wahanga wa kesi za udhalilishaji unavyosokota mioyo yao.
Makala

MAKALA: Ukosekanaji wa fidia  kwa wahanga wa kesi za udhalilishaji unavyosokota mioyo yao.

  NA THUREYA GHALIB- PEMBA. . Kuna Msemo usemao Adhabu ya kaburi aijuaje maiti  huu ni msemo unaofahamisha kuwa aliyefikwa na shida fulani ndiye  anaejua na kufahamu shida ya jambo husika. Au pia  kuna msemo unaosema  aisifuye mvua imemnyeshea,msemo huu unamana kuwa  kila jambo ambalo mtu analizingumzia atakuwa aidha  ana uzoefu nalo  kwa namna moja au nyengine analifahamu. Hii ni misemo inayonesha ni jisi gani Mtu anapopata matatizo unatakiwa umskilize na kumpa faraja maana yeye ndie mtu pekee anaehisi uchungu wa Jambo hilo. Leo Katika Makala haya nimelenga kuzungumzia ni kwa namna Gani ukosekanaji wa Fidia  kwa Wahanga wa Kesi za udhalilishaji unavosokota mioyo yao . Nini maana ya malipo ya fidia? Maana ya malipo ya fidia kikawaida  fidia inarejelea malipo ya pesa yanayot...
MAKALA: Ramia, mwanamke aliepambania kujengwa barabara ya Sebuwatu, lengo lake ijegwe kwa kiwango cha lami
Makala, Wanawake & Watoto

MAKALA: Ramia, mwanamke aliepambania kujengwa barabara ya Sebuwatu, lengo lake ijegwe kwa kiwango cha lami

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA  Kwa watu wa Sebuwatu, kati ya kijiji chao na mji wa Wete Pemba, ni mafupi sana… karibu kilomita tatu. Lakini muda ulikuwa unachukua muda mrefu kwa aliyetaka kwenda huko au kurudi kijini kutoka mji wa Wete. Kuifanya safari hio kwa miguu au gari la ng’ombe ni kazi pevu, yenye sulubu na huwa ngumu zaidi kwa mtu aliyebeba mzigo kichwani au mkononi. Kwa aina wajawazito ndio hatari kabisa, hiyo inatokana na njia kuwa mbaya sana na zaidi wakati wa mvua. Kila kukicha wanakijiji walikuwa wanajiuliza shida hii walioishuhudia tokea wakiwa wadogo itakwisha lini na wao kuwa na usafiri mzuri, wa haraka na salama kama wanavijiji wengine wa kisiwa cha Pemba? Tunaambiwa baada ya dhiki faraja na sasa matatizo waliokuwa nayo wanakijiji cha Sebuwatu ...