Tafiti zinaoesha kwamba wanawake wanafanya vizuri katika nafasi za uongozi licha ya changamoto zinazowakabili.
NA ZUHURA JUMA, PEMBA
“WANAWAKE wana uwiano mkubwa wa vipawa na uwezo wa kibinadamu kwenye kutambua mahitaji ya jamii, ila ushiriki wao ni mdogo kwenye vyombo vya kutoa maamuzi”, hayo ni maneno yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa umoja wa ulaya juu ya wanawake na uamuzi mwaka 1992.
Tafiti zinaoesha kwamba wanawake wanafanya vizuri katika nafasi za uongozi, kutokana na kwamba ni watu wa kutimiza ahadi, wanajitolea, hawapendi rushwa, ni waadilifu na wanaheshimu usawa wa kijinsia.
Wanawake wengi ambao ni viongozi wameleta mafanikio na kuwa mfano bora wa kuigwa, hilo ni jambo la faraja kuona maendeleo ambayo chanzo chake yanatokana na wanawake.
Miongoni mwa changamoto kubwa inayowakabili wanawake ni ufinyu wa uwezeshaji na uchache wa ushiriki katika vyombo muhimu vya ...