RAIS DK. MWINYI AHUDHURIA TAARAB MAALUM YA MIAKA 59 YA MAPINDUZI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi jana usiku alijumuika na wananchi na viongozi mbalimbali wa chama na serikali kwenye taarabu rasmi ya maadhimisho ya miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo.
Taarabu hiyo ilitumbuizwa na vikundi viwili tofauti kikiwemo kikundi cha sanaa cha taifa pamoja na kikundi cha “Island Morden taarabu, maarufu kama Wajelajela” ilikua maalumu kwa kuyaenzi Mapinduzi ya mwaka 1964 pamoja na kumpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kazi kubwa aliyoifanya ndani kipindi cha miaka miwili ya uongozi kwa kuiletea Zanzibar maendeleo makubwa.
Katika hafla hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Golden Tulip, Uwanja wa ndege, Zanzibar ulipambwa kwa vifijo na hoi...