“Tumieni kalamu zenu kutetea sheria ya habari zenye mapungufu” Shifaa Said
IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA
WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kutumia kalamu zao kufanya utetezi wa wa sheria ya habari zenye mapungufu ili zifanyiwe maboresho.
Akifungua mafunzo ya siku mbili katika Ofisi ya TAMWA Chake Chake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchechemuzi na utetezi kutoka TAMWA Shifaa Said Hassan alisema iwapo waandishi wataendelea kutumia kalamu zao vizuri kufanya utetezi wa sheria hizo, itasaidia kupata sheria zilizo bora na zisizonuima uhuru wa habari.
Alisema kuwa, zipo sheria za Usajili wa Wakala wa Habari na Magazeti na Vitabu nambari 5 ya mwaka 1988 ambayo imerekebishwa Sheria nambari 8 ya mwaka 1997 na ile sheria ya Tume ya Utangazaji nambari 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa maboresho nambari 1 ya mwaka 2010, ambazo baadhi ya vipen...