Monday, May 20

Sheria

“Tumieni kalamu zenu kutetea sheria ya habari zenye mapungufu” Shifaa Said
Sheria

“Tumieni kalamu zenu kutetea sheria ya habari zenye mapungufu” Shifaa Said

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kutumia kalamu zao kufanya utetezi wa wa sheria ya habari zenye mapungufu ili zifanyiwe maboresho. Akifungua mafunzo ya siku mbili katika Ofisi ya TAMWA Chake Chake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchechemuzi na utetezi kutoka TAMWA Shifaa Said Hassan alisema iwapo waandishi wataendelea kutumia kalamu zao vizuri kufanya utetezi wa sheria hizo, itasaidia kupata sheria zilizo bora na zisizonuima uhuru wa habari. Alisema kuwa, zipo sheria za Usajili wa Wakala wa Habari na Magazeti na Vitabu nambari 5 ya mwaka 1988 ambayo imerekebishwa Sheria nambari 8 ya mwaka 1997 na ile sheria ya Tume ya Utangazaji nambari 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa maboresho nambari 1 ya mwaka 2010, ambazo baadhi ya vipen...
Wamiliki wa vyombo vya habari wametakiwa kujisajili Tume ya Utangazaji.
Sheria

Wamiliki wa vyombo vya habari wametakiwa kujisajili Tume ya Utangazaji.

  Na Maryam Talib – Pemba.  Ofisa Mdhamin Wizara ya habari Vijana Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau amewataka wamiliki wa vyombo vya habari hususani  online tv wasajili vyombo vyao  Tume ya utangazaji kwa lengo la kuondosha shubha ama changamoto  zinazojitokeza katika kazi zao. Aliyasema hayo alipokuwa akifungua mapitio ya sheria ya tume utangazaji yaliyofanyika katika ukumbi wa uwezeshaji Gombani Kisiwani Pemba Mdhamini huyo alisema lengo la kufanya hivyo ni kuona vyombo vyote vinatoa taarifa zake kwa jamii iwe zinaendana na mazingira ya watu na endapo itatokezea  tatizo kwenye taarifa iwe ni wepesi kuelekezana na kurudi kwenye mstari kwani kila binadamu ana mapungufu yake. “Na nyinyi watu wa tume nawambia iwe basi mana kuna watu wengine wanadharau kuvunja ut...
POLISI KUZUWIA UHALIFU KIDIGITALI
Sheria

POLISI KUZUWIA UHALIFU KIDIGITALI

NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR  Kamishna wa Polisi Zanzibar CP. HAMAD KHAMIS HAMAD amesema Utendaji wa kusimamia Sheria wa Jeshi la Polisi lazima ubadilike kwa kujikita katika matumizi ya taaluma na vifaa vya kisasa ili kukabiliana na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia yanaoendana na mabadiliko ya ufanyaji wa uhalifu. Akifungua mafunzo ya Mfumo wa kutoa taarifa kidigitali, kwa Wakaguzi wa Shehia Mikoa ya Zanzibar, hapa Ukumbi wa Chuo cha Polisi Zanzibar amesema mafunzo hayo yatarahisisha upatikanaji wa taarifa za uhalifu haraka na kufanyiwa kazi kwa wakati. Nae Mrakibu wa Polisi Kutoka Makao Makuu ya Polisi Dodoma DKT. EZEKIEL KYOGO ameeleza kuwa Matumizi ya Technolojia kwa Watendaji wa Jeshi laPolisi ni muhimu na yatasaidia kutoa huduma bora za kipolisi kwa wananchi. ALI S...
TAMWA-Zanzibar yataka uwazi na mawasiliano yaendelee kwenye kesi za ukatili.
Sheria

TAMWA-Zanzibar yataka uwazi na mawasiliano yaendelee kwenye kesi za ukatili.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: TAMWA-Zanzibar yataka uwazi na mawasiliano yaendelee kwenye kesi za ukatili. CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kinaziomba taasisi zinazosimamia masuala ya sheria na upatikanaji wa haki likiwemo Jeshi la Polisi, Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na Mahakama kuendeleza uwazi na mawasiliano katika kushughulikia kesi za ukatili wa kijinsia ikiwemo mauaji. Hivi karibuni Mahakama Kuu Zanzibar ilitoa taarifa kuwa imemuhukumu mshitakiwa Haji Jaha Issa (37) kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kumuua kwa makusudi Hajra Abdallah Abdallah (21) ambapo alimchoma kisu kifuani, ubavuni na tumboni. Taarifa hiyo ilitaja kuwa hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Rabia Hussein Mohammed ambaye aliridhishwa na ushahidi uliotolewa katika mauaji hayo yal...
Wasaidizi wa sheria wafutiwa ada Zanzibar-Waziri Haroun
Sheria

Wasaidizi wa sheria wafutiwa ada Zanzibar-Waziri Haroun

  NA ABDI SULEIMAN, PEMBA. WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman, ametangaza rasmin kufuta ada ya usajili kwa wasaidizi wa sheria. Hayo aliyasema wakati akifunga jukwaa la tatu la mwaka la msaada wa kisheria huko katika ukumbi wa chuo cha utalii Maruhubi Unguja. Alisema ameamua kuondosha ada hiyo, ili kuwaondoshea gharama katika utendaji wao wa kuwasaidia wananchi katika changamoto zinazowakabili. Haroun alisema ufutaji wa ada hiyo, kwa sasa unawahusu watoa msaada wa kisheria wanaojisajili mmoja mmoja wakiwemo wasaidizi wa sheria, mawakili, mavakili na wanasheria ambao hujisajili kama watoa msaada wa kisheria. “Nafahamu kuwa wasaidizi wa sheria mnalipa ada ya shilingi 20,000 kuanzia sasa natangaza rasmin kuifuta ...