Sunday, March 26

Kitaifa

ZEMA yateketeza tani 1.5 ya vifuko vya plastiki Pemba vikiwa na thamani ya zaidi ya milioni 10
Kitaifa, MAZINGIRA

ZEMA yateketeza tani 1.5 ya vifuko vya plastiki Pemba vikiwa na thamani ya zaidi ya milioni 10

MAMLAKA ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA)Ofisi ya Pemba, leo 22/3/2023 imeteketeza vifuko vya plastiki tani 1.5 vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 10, mali ya mfanya biashara Mohamed Juma Ali mkaazi wa Kiuyu Minungwini. Vifuko hivyo vimeteketezwa katika  eneo la kwareni Vitongoji Wilaya ya chake Chake, baada ya mahakama Wilaya ya Wete kumtia hatiani na kuamuru kuteketezwa. Zoezi hilo la uteketezaji limeweza kushuhudiwa na viongozi mbali mbali wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  
“Serikali kuwapatia kifuta jasho wajumbe wakamati za Jamii za Shehia kwa kazi kubwa wanazozifanya”MKURUGENZI PEGAO
Kitaifa

“Serikali kuwapatia kifuta jasho wajumbe wakamati za Jamii za Shehia kwa kazi kubwa wanazozifanya”MKURUGENZI PEGAO

NA ABDI SULEIMAN. MKURUGENZI Mradi wa SWIL kutoka PEGAO Hafidh Abdi Said, amesema wakati umefika kwa wajumbe wakamati za Jamii za Shehia kutoka Wilaya Nne za Pemba, kuhakikisha zinapatiwa kifuta jasho serikalini kutokana na kazi kubwa wanazozifanya za kufatilia changamoto za shehia na kuweza kutatuliwa. Alisema kamati hizo zinafanya kazi ambazo zilipaswa kufanya na viongozi wa majimbo, Wilaya hata baadhi ya watendaji wa serikali, kwa lengo la kuwasaidia wananchi. Mkurugenzi huyo aliyaeleza hayo katika kikao kilichowakutanisha wajumbe wa kamati hizo, cha kuwasilisha ripoti zao za utekelezaji kupitia mradi wa SWIL kikao kilichofanyika Mjini Chake Chake. Alisema katika utekelezaji wa mradi huo, Pemba inaweza kuwa ya mfano kutokana na kazi zake kufanya kwa umakini na ufuati...
TAASISI ya Ifraji na Milele Zanzibar Foundation zawatupia jicho wanafunzi wa dahalia mwezi mtukufu wa Ramadhani
Kitaifa

TAASISI ya Ifraji na Milele Zanzibar Foundation zawatupia jicho wanafunzi wa dahalia mwezi mtukufu wa Ramadhani

NA ABDI SULEIMAN. WIZARA ya elimu na mafunzo ya amali Kisiwani Pemba, imepokea Msaada wa vyakula wenye thamani ya Tsh 33,618,000/- Kwa Skuli 16 zenye dahalia kutoka Kwa taasisi za Ifraj na Milele Zanzibar Foundation Kwa ajili ya mwezi mtukufu wa ramadhani. Skuli ambazo zimepatiwa Msaada huo ni pamoja na Madungu Sekondari, Fidel Castro, Dk, Salim Ahmed, Dk, Aman, CCK, Dk, Idrisa, Chasasa, Utaani, Pindua, Kengeja Ufundi, Amini Islamic,Vitongoji VTC,Daya VTC, Istiqama pamoja na Ambasha. Akipokea Msaada huo huko katika Ofisi za Milele Foundation, Ofisa Mdhamini wa Wizara ya elimu na mafunzo ya amali Pemba Mohammed Nassor alieleza kuwa amefarajika sana Kupata Msaada huo kwani umekuja muda muafaka. Ofisa huyo alifahamisha kuwa jambo ambalo wamelifanya taasisi hizo ni kitendo ch...
WAZIRI CHANDE AKABIDHI GARI KWA POLISI  MKOA WA KASKAZINI PEMBA.
Kitaifa

WAZIRI CHANDE AKABIDHI GARI KWA POLISI MKOA WA KASKAZINI PEMBA.

SAID ABRAHMAN—PEMBA. NAIBU Waziri wa fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kojani Hamad Hassan Chande amekabidhi gari yenye thamani ya Tsh milioni 160 kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba. Akikabidhi gari hilo huko katika kituo cha Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, alisema kuwa hiyo ni ahadi yake kwa jeshi hilo  ambayo aliiweka. Chande alilitaka jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba  kulitunza gari hilo kwa namna yeyote ile ili liweze kuwasaidia katika harakati zao za kila siku. Alifahamisha kuwa hiyo ni mwanzo tu kwani baada ya kumalizika kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajia kutoa gari 3 aina ya Noha kwa jeshi la Polisi, KMKM Kojani pamoja na Chuo cha Mafunzo Kangagani. "Ninamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano ...
Mkurugenzi TAMWA-ZNZ ataka Asasi za kirai zijitathmini
Kitaifa

Mkurugenzi TAMWA-ZNZ ataka Asasi za kirai zijitathmini

Asasi za kiraia Zanzibar (CSOs) zimetakiwa kujiwekea utaratibu maalumu  wa kujipima kila baada ya kipindi cha miezi mitatu kwa lengo la kujitathmini na kutambua njia bora za kufikia malengo yao. Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa wakati alipokua  akizungumza na baadhi ya wawakishi wa asasi 30 kutoka Unguja na Pemba katika mkutano uliofanyika kwenye umbi wa Chama hicho Tunguu wilaya ya kati Unguja. Alisema Asasi za kiraia zina mchango mkubwa wakuleta mabadiliko kwenye jamii, hivyo wana wajibu wa kujiewekea utaratibu maalumu ambao utawapa fursa wahusika kujitathmini na kujua wapi walipo na wanataka kufanya nini. Alisema ili Asasi hizo ziweze kuendelea kufanya kazi zao kwa maslahi ya jamii wanapaswa kuacha kufanya  kazi kwa mazoea wakiamini kuwa kila kitu ni...