Friday, September 29

Kitaifa

Huduma za kimtandao changamoto upatikanaji wa Vyeti vya kuzaliwa.
Kitaifa

Huduma za kimtandao changamoto upatikanaji wa Vyeti vya kuzaliwa.

Baadhi ya wazazi wamelalamikia   kukosa huduma za vyeti vya  kuzaliwa vya watoto wao katika kituo cha  utolewaji wa huduma  hizo wilaya  ya Chake chake  kwa zaidi ya siku 5 kwa  kile wanachojibiwa na watoa huduma kuwa ni  kukosekana kwa huduma ya kimtandao katika ofisi ya wakala wa usajili wa  matukio ya huduma za kijamii. Hayo wameyabainisha wazazi hao kwa nyakato tofauti wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyefika eneo la tukio na kukumbana na wazazi hao.  Wamesema  suala hilo limekuwa likisababisha hasara kwao kutokana na kutoka masafa ya mbali  huku mchezo huo wa nenda rudi   ukikosa  kwa zaidi ya siku nne sasa  ambao  wanasema hofu yao ni kucheleweshewa na  baadae kutozwa  malipo katika huduma hiyo kwa kosa la kuchelewesha.  Aidha wanachoendelea kulalamikia ba...