Friday, June 2

Wanawake & Watoto

Dk. Mwinyi Ameitaka Kamati ya Kuzuia Udhalilishaji wa Kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Dk. Mwinyi Ameitaka Kamati ya Kuzuia Udhalilishaji wa Kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameiagiza kamati ya kuzuia udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema na kwenye mwelekeo wa uhuru wa matumizi hayo kwa Zanzibar. Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye hafla ya uzinduzi wa kamati ya kuzuia udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar huko ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakili, Kikwajuni Wilaya ya mjini. Alisema, mitandao inapotumiwa vibaya ni kishawishi kimojawapo cha mmong’onyoko wa maadili na vitendo vya udhalilishaji.  “Naiagiza Kamati hii ifanye kazi ya kuchunguza athari za matumizi ya mitandao ya kijamii na ongezeko la kesi za udhalilishaji, baada ya kufanya kazi hiyo, itoe ushauri na mapendekezo Serikalini ili tuwe na muel...
Wanawake wenye nia ya kugombea Uchaguzi mkuu 2025 watakiwa kujifunza kwa waliowatangulia
Siasa, vijana, Wanawake & Watoto

Wanawake wenye nia ya kugombea Uchaguzi mkuu 2025 watakiwa kujifunza kwa waliowatangulia

NA MWANDISHI WETU. KATIKA kuhakikisha ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi unaongezeka, wanawake wenye ndoto za kugombea uongozi wameshauriwa kuanza kujifunza kutoka kwa wanawake wanasiasa waliowatangulia ili kuongeza ujasiri na uthubutu wa kukabiliana na vikwazo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025. Ushauri huo umetolewa na wanasiasa wanawake wakongwe katika mkutano wa jukwaa la wanawake na uongozi lililoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari WanawakeTanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) na Ubalozi wa Norway kwa lengo la kuwaunganisha wanawake wanasiasa kutoka vyama mbalimbali vya siasa Pemba kubadilishana uzoefu na kuwajengea uwezo kuhusu ushiriki wao kwenye nafasi za uongozi na namna ya kukabiliana na vikwazo vinavyoweza kurejesha nyuma ufikiaji wa malengo ya wanawake kiuongoz...
Mkurugenzi TAMWA-ZNZ atoa wito kwa wanawake kuelekea uchaguzi mkuu 2025
Kitaifa, Wanawake & Watoto

Mkurugenzi TAMWA-ZNZ atoa wito kwa wanawake kuelekea uchaguzi mkuu 2025

Ikiwa imesalia miaka miwili wananchi wa Tanzania kutekeleza haki yao ya kikatiba kuchagua na kuchaguliwa kupitia uchaguzi mkuu mwaka 2025 Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa amewataka wanawake wenye nia za kugombea kutokubali kutumiwa na wenye ajenda zao, zikiwemo za kukwamisha wanawake kutoshika nafasi za uongozi. Aliyasema hayo  wakati alipokua akizungumza na wanawake  kutoka vyama mbali mbali vya siasa Zanzibar  katika ofisi za chama hicho Tunguu Wilaya ya kati Unguja. Alisema  licha ya kuwa Zanzibar ina idadi kubwa ya wanawake wengi zaidi lakini kwa mshangao mkubwa bado wanawake hao  hawapati nafasi ya kuchaguliwa kutokana na kasoro mbali mbali zikiwemo za mitazamo hasi iliokua ikitawala kwenye jamii. Alieleza kuwa ili wanawake welio wengi waweze kufanikiwa kwenye uchaguz...
Vitisho kutoka kwa wagombea wenzao ni changamoto kubwa inayowarudisha nyuma wanawake  kuwania nasafi za uongozi
Siasa, Wanawake & Watoto

Vitisho kutoka kwa wagombea wenzao ni changamoto kubwa inayowarudisha nyuma wanawake  kuwania nasafi za uongozi

NA ABDI SULEIMAN. WANAWAKE watiania wamesema moja ya changamoto kubwa inayowarudisha nyuma kuwania nasafi za uongozi katika changuzi mbali mbali zinazofanyika ni uwepo wa vitisho wanavyokumbana navyo kutoka kwa wagombea wenzao. Wamesema vitisho hivyo huwafika wao, pamoja na familia zao na wakati mwengine wagombea hao huwafuata wazazi wao au waume zao ili kukatazwa kuachia nafasi hiyo aliyogombea. Wakichangia mada mbali mbali wakati wa mafunzo ya siku mbili yaliyoandaliwa na Jumuiya ya PEGAO, kwa Wanawake wanaotarajiwa kugombea nafasi za uongozi na siasa katika mchakato wa Kidemokrasia Kisiwani Pemba, ikiwa ni utekelezaji wa mradi SWILL, unatekelezwa kwa pamoja kati ya TAMWA  Zanzibar, ZAFELA na PEGAO kwa ufadhili wa Ubalozi wa Norway nchini. Mmoja ya watia nia hao Asha Ali...