Monday, May 20

Wanawake & Watoto

Wajumbe wa bodi ya Jukwaa la haki za watoto wakutana kisiwani Pemba kujadili mpango kazi mpya.
Wanawake & Watoto

Wajumbe wa bodi ya Jukwaa la haki za watoto wakutana kisiwani Pemba kujadili mpango kazi mpya.

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA MRATIBU wa Jukwaa la haki za Watoto Zanzibar Sohpia Leghela, alisema lengo la mkutano mkuu wa bodi ya ushauri ya Watoto Zanzibar ni kuwaleta Watoto pamoja kuweza kujadiliana na kutoka na mpango kazi wa mwaka 2024/2025.   Mratibu huyo aliyaeleza hayo wakati akifungua mkutano huo, uliowashirikisha wajuumbe wa bodi hiyo kutoka Unguja na Pemba, na kufanyika mjini Chake Chake. Alisema katika mkutano huo, mapendekezo ambayo watoto wameweza kuyatoa ni pamoja na kutoa elimu juu ya haki za Watoto, kwa Watoto wenyewe pamoja na kufika kwa jamii. Alisema ni kufika kwa jamii na kuelezea umuhimu wa mabaraza ya Watoto, pamoja na kukutana na viongozi wa serikali, hasa ngazi ya wilaya kujadiliana nao namna gani wanaweza kuyawezesha mabaraza ya watoto ngazi ya Wilaya...
WATU WENYE ULEMAVU PEMBA: “BADO HAKI ZETU ZINAPIGWA MATEKE’’
Wanawake & Watoto

WATU WENYE ULEMAVU PEMBA: “BADO HAKI ZETU ZINAPIGWA MATEKE’’

NA HAJI NASSOR, PEMBA WATU wenye ulemavu kisiwani Pemba, wamesema bado wanamashaka na utekelezaji wa haki zao, ikiwemo ajira, miundombinu ya kuyafikia majengo ya umma na upatikanaji huduma za kijamii kwa ina ya mazingira yao. Walisema, wamekuwa na watetezi wengi mno katika taifa, lakini kwenye utekezaji halisi, wanaendelea kukumbana na vikwazo, hali inayosababisha kuwavunja moyo, kwa baadhi ya wakati. Hayo waliyasema Novemba 27, 2023 kwenye kongamano la siku moja, lililoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ na kufanyika ofisi ya Umoja wa Watu Wenye Ulemavu ‘UWZ’ Mkanjuni, ikiwa ni muendelezo wa mikutano, ya ndani ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji. Walisema, hadi miaka ya hivi karibuni, yapo majengo ya umma yanajengwa bila ya ...
“Ni vyema kuzitumia siku 16 kwa kujadili na kutafakari namna ya kuongeza juhudi katika mapambano ya ukatili wa kijisnia”-Bibi Jeanne  Clark
Kitaifa, Wanawake & Watoto

“Ni vyema kuzitumia siku 16 kwa kujadili na kutafakari namna ya kuongeza juhudi katika mapambano ya ukatili wa kijisnia”-Bibi Jeanne  Clark

NA KHADIJA KOMBO-PEMBA. Wadau katika mapambano dhidi ya Vitendo vya Udhalilishaji wametakiwa kuongeza juhudi katika kuvifichua vitendo hivyo ili viweze kuchukuliwa hatua na kukomeshwa kabisa ndani ya jamii. Wito huo umetolea na Bibi Jeanne  Clark kutoka Ubalozi wa Marekani wakati alipokuwa akizungumza na wadau hao ikiwa ni pamoja na  wanasheria kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashkata , Maafisa wa Jinsia, wanaharakati kutoka Jumuiya ya Waandishi wa habari   Tanzania  Tamwa pamoja na wanafunzi kutoka Skuli za Madungu na Chuo cha Mwalim nyerere na Utumishi wa Umma  Kisiwani Pemba huko katika Ukumbi wa maktaba ya American Conner Chake Chake   ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji wa kijinsia. Amesema Udhalilishaji una maana pana hiv...
TAMWA ZANZIBAR yakemea udhalilishaji wa watoto kupitia mitandao ya kijamii.
Kitaifa, vijana, Wanawake & Watoto

TAMWA ZANZIBAR yakemea udhalilishaji wa watoto kupitia mitandao ya kijamii.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: TAMWA ZANZIBAR yakemea udhalilishaji wa watoto kupitia mitandao ya kijamii. CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA –ZNZ) kinaiasa jamii kujizuia kurikodi watoto wadogo na kuwaweka katika mitandao baada ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji kwani kufanya hivyo ni kuwadhalilisha zaidi. Kufuatia kuenea kwa simu janja/mtetemo kumeibuka watu ambao wanarikodi watoto na kusambaza taarifa zao kupitia picha, sauti na video kinyume na taratibu na maadili ya uandishi wa habari. Tunaamini kwamba watu hawa wana nia njema ya kutaka haki itendeke na kuwatia ujasiri zaidi watoto lakini tunashauri wasifanye kazi hiyo na badala yake wawaaachie waandishi wa habari ambao wamesomea kazi hiyo na hivyo wanajua kuficha utambulisho wa watoto hao. Wato...

Warning: file_get_contents(): http:// wrapper is disabled in the server configuration by allow_url_fopen=0 in /data/40/5/71/99/5397425/user/6768456/htdocs/portal/wp-content/plugins/xt-visitor-counter/xt-visitor-counter.php on line 48

Warning: file_get_contents(http://api.xtrsyz.org/xt-visitor-counter/default.php?domain=www.pembapress.club&time=1716223605): failed to open stream: no suitable wrapper could be found in /data/40/5/71/99/5397425/user/6768456/htdocs/portal/wp-content/plugins/xt-visitor-counter/xt-visitor-counter.php on line 48