MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE AACHIWA HURU
Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu, leo Machi 4, 2022 wamefutiwa mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakabili katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.
Mbowe na wenzake wameachiwa baada ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali, DPP, kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo hatua ambayo imepelekea Mbowe na wenzake watatu kuachiliwa huru mara moja.
Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ilikuwa imemshikilia Mbowe na wenzake watatu kwa kesi ya kujibu kuhusiana na tuhuma mbalimbali zikiwemo za kupanga njama za kufanya vitendo vya kigaidi.
Taarifa ya kuondoa mashtaka iliwasilishwa na wakili wa serikali. “Mheshimiwa Jaji Taarifa Hii tunaiwasil...