Monday, May 20

Siasa

Mwenyekiti   UWT  Taifa afanya ziara Kisiwani Pemba, amekagua miradi mbali mbali ya maendeleo
Siasa

Mwenyekiti   UWT  Taifa afanya ziara Kisiwani Pemba, amekagua miradi mbali mbali ya maendeleo

NA AMINA AHEMD-PEMBA. MWENYEKITI wa umoja wa wanawake  UWT  Taifa   Mery Pius Chatanda amepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Dr. Hussein Ali Mwinyi  ya kujenga miradi mikubwa ya Maendeleo  kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba na kueleza Ilani ya CCM anaekeleza kwa kasi kubwa mno ambayo   haikuwahi kutokea. Akizungumza kwa nyakati tofauti Mwenyekiti huyo wa UWT  amempongeza Rais  Dkt Mwinyi  pamoja na Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Dr. Samia Suluhu Hassan  kwa juhudi   za kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi  na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo kwa wananchi ndani ya mkoa huo. Amesema kasi ya  ujenzi wa maendeleo katika miradi  iliyomo ndani ya mkoa huo itasaidia kuongeza zaidi uhai wa chama na jumuiya zake  sambamba na kuendelea kuwatumiki...
MAKALA MAALUM: MWANAMKE ALIEACHA ALAMA ZA MAENDELEO ZINAZOWASAIDIA WANANCHI.
Makala, Siasa

MAKALA MAALUM: MWANAMKE ALIEACHA ALAMA ZA MAENDELEO ZINAZOWASAIDIA WANANCHI.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA. KATIKA maisha watu huacha kumbukumbu ambazo wakiwa hawapo katika ajira au wamehamia eneo jengine hukumbukwa kwa vile huacha alama za maendeleo zisiofutika. Kwa watu  wa jimbo la Chonga na vitongoji vyake ikiwemo Pujini na kwengineko kisiwani Pemba, mchango wa maendeleo katika maeneo yao  uliotolewa na aliyekuwa Mbunge wa kuteuliwa wa jimbo hilo kutoka mwaka 1985 hadi 1990 , Bibi Lela  Nassor Khamis, hautasahaulika. Mbunge huyu mstaafu, ambaye umri wake sasa ni miaka 71,  hivi sasa anakaa Chanjaani, mjini Chake Chake,bado harakati zake za kukiletea maendeleo kisiwa cha Pemba huzungumzwa kwa kutolewa mfano bora wa kiongozi mwanamke katika jamii. Wakati alipokuwa mbunge wa Chonga Bi Lela alizikuta changamoto nyingi zikiwakabili wananchi wa jimbo hilo na kupun...
MADARAKA NI AMANA – MHE. OTHMAN
Siasa

MADARAKA NI AMANA – MHE. OTHMAN

Makamu Mwenyekiti wa ATC-Wazalendo Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman amesema dhana ya mageuzi ni uwanja mpana, ambapo utekelezaji wake ni kutoka mbali, kuanzia Chaguzi za haki na demokrasia ndani ya Chama. Mheshimiwa Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo leo katika Mkutano Maalum wa Viongozi Wapya wa Chama hicho, kutoka Mikoa ya Wete na Micheweni kichama, huko katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Bopwe-Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema kuwa Chama hicho ni taasisi inayosimamia harakati za kuleta mageuzi ya kisiasa na ili hatimaye kuongoza Nchi, hivyo ni wajibu wa kila kiongozi kuanza na mabadiliko ya nafsi yake, kwa kuzingatia misingi ya uadilifu, haki, kuvumiliana, umoja na mashirikiano mbele ya wananchi wote. Akiongelea...
Viongozi wa ACT Wazalendo watakiwa kuelewa dhima waliyonayo
Siasa

Viongozi wa ACT Wazalendo watakiwa kuelewa dhima waliyonayo

  Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman ametoa wito kwa Viongozi wa Ngazi mbalimbali kuelewa dhima waliyonayo ili kuhakikisha Watu wote wa Nchi hii wanarudisha Imani ya kuishi kwa heshima na matumaini. Mheshimiwa Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo leo katika Mkutano Maalum wa Viongozi Wapya wa Chama hicho wa ngazi ya Majimbo na Matawi, kutoka Mikoa ya Chake Chake na Mkoani kichama, huko katika Ukumbi wa Samael Gombani, Mkoa wa Kusini Pemba. Amesema kuwa lazima Safu za Viongozi Wapya wa Chama hicho zijipange na zijitathmini kwa udhati kwa kuzingatia haja ya kutumikia umma wa watu wa Nchi hii, kwa misingi ya Amani, umoja, utulivu, maridhiano na mshikamano, pamoja na kuzingatia dhima ya kuivus...
CCM YAKIRI UMUHIMU WA RIPOTI YA APRM KWA WANANCHI NA SERIKALI
Siasa

CCM YAKIRI UMUHIMU WA RIPOTI YA APRM KWA WANANCHI NA SERIKALI

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Mhe. Mohammed Said Mohammed (DIMWA) amesema kuwa mpango wa APRM Tanzania kuitathmini Serikali kwa vigezo vya Utawala Bora ni mzuri na unahitajika sana kuungwa mkono kwavile unalenga moja kwa moja kubaini changamoto zilizopo katika jamii na kuzitafutia suluhisho lake ili Serikali iweze kuleta ustawi mzuri kwa wananchi. Hayo ameyasema leo hii wakati alipokutana na viongozi wa APRM Tanzania waliofika Ofisini kwake Kiswandui kwa lengo la kujitambulisha pamoja na kuelezea mikakati ya kuelekea Ripoti ya Pili ya Tathmini ya masuala ya Utawala Bora Tanzania. Mhe. Dimwa amesema kuwa utaratibu wa kujitathmini unatumika pia katika Chama cha Mapinduzi kuangalia kwa namna gani wameweza kutekeleza Ilani ya Chama hivyo Ripoti ya Tathmini ya Utawala Bora ya APRM...