Friday, June 2
Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na waumini wa Masjid Riyaadh Amani katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.
DINI

Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na waumini wa Masjid Riyaadh Amani katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na waumini wa Masjid Riyaadh Amani katika Ibada ya Sala ya Ijumaa. Akiwasalimia waumini hao Alhajj Hemed amewataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kupinga vitendo viovu nchini ambavyo vinamchukiza Allah (S.W) na kuondoa taswira ya Zanzibar. Amesema zipo njia nyingi zinazopelekea kuongezeka kwa vitendo hivyo ikiwemo kuwakaribisha watu tusiowajua dhamira na malengo yao, ambao pia  tunashirikiana nao katika harakati za kila siku. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema ulimwengu umetawaliwa na utandawazi hivyo, ni vyema kusimamia misingi ya Dini ya Uislamu katika maisha yetu ili kupunguza athari zitokanazo na utandawazi huo. Sambamba na hayo Mhe. Hemed ameeleza kuwa Serikali inaendelea na uj...
Dk. Mwinyi Ameitaka Kamati ya Kuzuia Udhalilishaji wa Kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Dk. Mwinyi Ameitaka Kamati ya Kuzuia Udhalilishaji wa Kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameiagiza kamati ya kuzuia udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar, iangalie suala la matumizi na athari za mitandao kwa vijana ili serikali ijipange vyema na kwenye mwelekeo wa uhuru wa matumizi hayo kwa Zanzibar. Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye hafla ya uzinduzi wa kamati ya kuzuia udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar huko ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakili, Kikwajuni Wilaya ya mjini. Alisema, mitandao inapotumiwa vibaya ni kishawishi kimojawapo cha mmong’onyoko wa maadili na vitendo vya udhalilishaji.  “Naiagiza Kamati hii ifanye kazi ya kuchunguza athari za matumizi ya mitandao ya kijamii na ongezeko la kesi za udhalilishaji, baada ya kufanya kazi hiyo, itoe ushauri na mapendekezo Serikalini ili tuwe na muel...
UTPC  imeendesha kikao kazi maalumu na waratibu wa klabu.
Kitaifa

UTPC imeendesha kikao kazi maalumu na waratibu wa klabu.

UTPC jana imeendesha kikao kazi maalumu na waratibu wa klabu za waandishi wa habari nchini kikiwa na lengo la kufanya ufuatiliaji wa mambo yaliyokubaliwa katika vikao vilivyopita ambayo kimsingi ni kuboresha utendaji wa klabu za waandishi wa habari ili kufikia dira ya kuitoa UTPC mahali pazuri na kuipeleka pazuri zaidi (Moving UTPC from Good to Great) Pamoja na mambo mengine, kikao kazi hicho kilijadili shughuli zilitelelezwa na klabu za waandishi wa habari nchini katika kipindi cha mwezi Aprili hadi Mei 2023 lakini pia kueleza mipango iliyopo kwa kipindi cha mwezi Juni 2023. Hata hivyo, Mkurugenzi wa UTPC Bw. @kennethsimbaya ametumia fursa hiyo kuziomba Klabu za waandishi wa habari kuwasimamia vizuri waandishi wa habari ili kutimiza adhima ya vyombo vya habari ya kuwa sauti ya ...
Wadau wakutana kupitia rasimu ya  uchambuzi wa hali halisi ya sera ya msaada wa kisheria ya mwaka 2017.
Sheria

Wadau wakutana kupitia rasimu ya uchambuzi wa hali halisi ya sera ya msaada wa kisheria ya mwaka 2017.

  NA ABDI SULEIMAN. AFISA Mdhamini Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria Utumishi na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali, amesema lengo la kukusanya maoni ya Rasimu ya Uchambuzi wa hali halisi ya sera ya msaada wa Kisheriaya Mwaka 2017, ni kwenda sambamba na mabadiliko ya dunia katika utoaji wa msada wa kisheria kwa wananchi. Alisema hivi sasa mambo mengi yamebadilika hivyo na watoa msaada wakisheria wanapaswa kubadilika katika utoaji wa elimu ya msaada wa kisheria kwa wananchi, kwa kuhakikisha hata vijijini wananchi wanapatiwa elimu hiyo. Hayo aliyaeleza wakati akifungua mkutano wa wahusika (wadau) wa kukusanya maoni ya Rasimu ya Uchambuzi wa hali halisi ya sera ya msaada wa Kisheriaya Mwaka 2017, mkutano uliofanyika mjini chake chake. Alisema sera hiyo itaka...
Dk. Hussein  Mwinyi azindua tena Kamati ya Maridhiano baina ya Chama cha Mapinduzi na ACT Wazalendo.
Kitaifa, Siasa

Dk. Hussein Mwinyi azindua tena Kamati ya Maridhiano baina ya Chama cha Mapinduzi na ACT Wazalendo.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameendelea kusisitiza dhamira yake njema ya kuiunganisha tena Zanzibar kuwa moja yenye amani, upendo, maridhiano na mshikamo. Ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozindua tena Kamati ya Maridhiano baina ya Chama cha Mapinduzi na ACT Wazalendo ifanyekazi pamoja kuendeleza amani iliyopo nchini. Alisema bado ana nia ya kuiendeleza Zanzibar kuwa moja bila kujali rangi, asili, imani za dini, au itikadi za kisiasa kama alivyoahidi kwa mara ya kwanza alipohutubia Baraza la Wawakilishi mwezi Novemba, 2022 juu ya dhamira yake ya kuwaunganisha wananchi wa Zanzibar kuwa wamoja. Alisema mara baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 waliendeleza tena Serikali ya Umoja wa kitaifa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar kama il...