Monday, May 20
Nchi za Afrika Mashariki zimekumbwa na tatizo kubwa la mtandao
Kimataifa

Nchi za Afrika Mashariki zimekumbwa na tatizo kubwa la mtandao

Muunganisho wa intaneti ulitatizwa ndani na karibu na mataifa kadhaa ya Afrika Mashariki siku ya Jumapili, shirika la uchunguzi wa mtandao la Netblocks lilisema, na kuongeza kuwa tukio hilo lilihusishwa na kushindwa kuathiri mifumo ya kebo ya SEACOM na EASSy chini ya bahari. Tanzania na kisiwa cha Ufaransa cha Mayotte vilikuwa na athari kubwa kwenye muunganisho wa intaneti, wakati Msumbiji na Malawi zikiona athari ya wastani, Netblocksā€™ ilisema kwenye jukwaa la mtandao wa kijamii la X (Zamani ikiitwa twitter). Kampuni ya mtandao ya Cloudflare ilisema kwenye moja ya akaunti zake za X inayofuatilia mwenendo kuwa kukatika kwa intaneti kunaendelea nchini Tanzania, Malawi, Msumbiji na Madagascar kutokana na hitilafu zilizoripotiwa kwenye Mfumo wa Kebo za Nyambizi wa Afrika Mashariki ...
Benki ya Exim Yaunga Mkono Jitihada za Rais Mwinyi, Wadau Kuchochea Kasi ya Utalii Zanzibar.
Biashara, UTLII

Benki ya Exim Yaunga Mkono Jitihada za Rais Mwinyi, Wadau Kuchochea Kasi ya Utalii Zanzibar.

Na Mukrim Mohammed Benki ya Exim Tanzania imesisitiza dhamira yake kuhudumia wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ndani na nje ya nchiĀ  ili kuunga mkono na kwenda sambamba na kasi pamoja na dhamira ya serikali katika kuchochea ukuaji wa sekta hiyo muhimu. Afisa Mtendaji wa Benki ya Exim Bw Jaffari Matundu alitoa ahadi hiyo mbele ya Raisi wa Zanzibar Dr. Hussein Mwinyi alipotembelea banda la benki hiyo kwenye Mkutano wa pili wa wadau wa sekta utalii Zanzibar (Z -Summit) unaofanyika visiwani humo hii leo. Kwa mujibu wa Bw Matundu, kufuatia jitihada mbalimbali zinazoendelea kufanywa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kuendeleza sekta ya utalii, Benki ya Exim imewekeza zaidi katika kuwahudumia wadau wa sekta hiyo ili waweze kunufaika na jitihada hizo za serikali kupitia hudum...
“Tumieni kalamu zenu kutetea sheria ya habari zenye mapungufu” Shifaa Said
Sheria

“Tumieni kalamu zenu kutetea sheria ya habari zenye mapungufu” Shifaa Said

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kutumia kalamu zao kufanya utetezi wa wa sheria ya habari zenye mapungufu ili zifanyiwe maboresho. Akifungua mafunzo ya siku mbili katika Ofisi ya TAMWA Chake Chake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchechemuzi na utetezi kutoka TAMWA Shifaa Said Hassan alisema iwapo waandishi wataendelea kutumia kalamu zao vizuri kufanya utetezi wa sheria hizo, itasaidia kupata sheria zilizo bora na zisizonuima uhuru wa habari. Alisema kuwa, zipo sheria za Usajili wa Wakala wa Habari na Magazeti na Vitabu nambari 5 ya mwaka 1988 ambayo imerekebishwa Sheria nambari 8 ya mwaka 1997 na ile sheria ya Tume ya Utangazaji nambari 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa maboresho nambari 1 ya mwaka 2010, ambazo baadhi ya vipen...