Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na waumini wa Masjid Riyaadh Amani katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na waumini wa Masjid Riyaadh Amani katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Akiwasalimia waumini hao Alhajj Hemed amewataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kupinga vitendo viovu nchini ambavyo vinamchukiza Allah (S.W) na kuondoa taswira ya Zanzibar.
Amesema zipo njia nyingi zinazopelekea kuongezeka kwa vitendo hivyo ikiwemo kuwakaribisha watu tusiowajua dhamira na malengo yao, ambao pia tunashirikiana nao katika harakati za kila siku.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema ulimwengu umetawaliwa na utandawazi hivyo, ni vyema kusimamia misingi ya Dini ya Uislamu katika maisha yetu ili kupunguza athari zitokanazo na utandawazi huo.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed ameeleza kuwa Serikali inaendelea na uj...