Wanawake wanaweza, watizameni kwa jicho la maendeleo
Imeandikwa na Amina Ahmed – Pemba
Walio Wengi wanafikiria ya kuwa mwanamke hawezi kusimama na kugombea nafasi ya uwongozi katika jimbo iwe ya Uwakilishi, Ubunge Udiwani na nyadhifa nyengine lakini, Kuelekea Uchaguzi Mkuu October 28 mwaka huu 2020 baadhi ya wanawake wameweza kuonesha ujasiri wa kugombea nafasi za uongozi majimboni licha ya awali kukabiliwa na changamoto ya virusi vya korona huku ikiwa ni mara ya kwanza kuingia katika mchakato wa kugombea .
Leo katika makala hii maalum ya wanawake na uongozi tutamuangalia mjasiriamali mwanamke alieamua kujitosa katika Nyanja ya kisiasa na kufanikiwa kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo la chake chake Mkoa wa kusini Pemba kupitia chama cha cha wakulima AAFP.
Ni Fatma Doto Shauri Mkaazi wa Madungu chake chak...