Friday, May 10
Wananchi wanaombwa kushiriki katika zoezi la uendelezaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura.
Kitaifa

Wananchi wanaombwa kushiriki katika zoezi la uendelezaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura.

  PICHA NA BAKAR MUSSA,PEMBA. BAKAR MUSSA, PEMBA Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Zanzibar,Jaji George Joseph Kazi amewataka wananchi na Viongozi wa vyama vya Siasa Kisiwani Pemba kushirikiana na Tume hiyo katika zoezi la uendelezaji wa Daftari la kudumu la wapigakura linalotarajiwa kuanza tarehe 2/12 mpaka tarehe 15 January 2024. Akitowa wito huo huko katika ukumbi wa kiwanda cha Makonyo Wawi Pemba wakati akifungua mkutano wa Wadau wa Uchaguzi Pemba juu ya Tume hiyo kufanya zoezi hilo litakalowawezesha wapiga kura wapya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao. Alisema uendelezaji wa Daftari la kudumu la wapigakura linalotarajiwa kuanza katika wilaya ya Micheweni na kumalizika katika wilaya ya Mkoani ni kwa mujibu wa sheria za Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC...
TIMU ya wanaume wa Mabadiliko Wilaya ya Mkoani, wameiyomba serikali nyumba ya kurekebisha tabia kwa watoto wanaokinzana na sheria.
Kitaifa

TIMU ya wanaume wa Mabadiliko Wilaya ya Mkoani, wameiyomba serikali nyumba ya kurekebisha tabia kwa watoto wanaokinzana na sheria.

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA   TIMU ya wanaume wa Mabadiliko Wilaya ya Mkoani, wameiyomba serikali kupitia Wizara husika, kuhakikisha ndani ya Kisiwa cha Pemba inajengwa nyumba ya kurekebisha tabia kwa watoto wanaokinzana na sheria. Hayo yameelezwa na mwenyekiti wa timu hiyo, ambae Pia ni Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria Wilaya ya Mkoani Nassor Hakim, wakati akichangia katika mkutano maalumu, ulioandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na kufanyika ofisi za Mkuu wa Wilaya Mkoani. Alisema kuwepo kwa nyumba hiyo ingesaidia watoto wanaokinzana na sheria, kwani wangeweza kuweka huko hata akitoka mtoto tayari ameshajifunza tabia njema. “Mtoto anapofanya kosa saivi anatakiwa kuadabishwa, lakini kwa vile nyumba hiyo unaona wazazi wanalipa ...
EJAT  imeondosha   makundi 5 ya  habari  katika mashindano hayo kwa mwaka huu wa 2023.
Kitaifa

EJAT  imeondosha  makundi 5 ya habari katika mashindano hayo kwa mwaka huu wa 2023.

NA FATMA HAMAD -  DODOMA. Kamati ya mandalizi ya Tunzo za Umahiri za Wandishi wa habari Tanzania EJAT imeondosha kundi la habari za Sensa, Habari za Gesi, Mafuta na Uchimbaji Madini pamoja na habari za Sayansi na Teknolojia katika mashindano hayo kwa mwaka huu wa 2023. Akizungumza na Wandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali katika mafunzo malumu ya uwandishi wa Habari za haki za binadamu Mwenyekiti wa kamati ya mandalizi wa Ijati ya mwaka 2023 Kajubi Mukajanga  huko Dodoma Tanzania Bara. Alisema kamati hiyo imeondosha Tunzo  hizo kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo kukosekana kwa habari zinazoshindaniwa kwenye kundi hilo. Aliendelea kusema licha ya kuondolewa kwa makundi hayo Bali kuna makundi mawili mapya yameongezwa ikiwemo Habari za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ...
ZAIDI YA MIFUGO 340 NA TREKA MOJA YAKAMATWA NDANI YA HIFADHI YA TAIFA RUAHA
hifdhi na utalii

ZAIDI YA MIFUGO 340 NA TREKA MOJA YAKAMATWA NDANI YA HIFADHI YA TAIFA RUAHA

Na. Jacob Kasiri - Ruaha. Mifugo ipatayo 345 na Trekta moja imekamatwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Ruaha na askari wa hifadhi hiyo waliokuwa doria  wakitekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi za Taifa  Tanzania Sura ya 282 marejeo ya mwaka 2002. Swala la uingizwaji wa mifugo na kilimo ndani ya Hifadhi ya Taifa Ruaha limekuwa ni tatizo sugu licha ya wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo kupewa elimu inayohusiana na madhara na kadhia inayoweza kulikumba Taifa kutoka na uharibifu wa ardhi Oevu ya Ihefu ambayo ni chanzo cha maji yanakwenda kuzalisha umeme katika mabwawa ya kimkakati nchini. Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Godwell Meng’ataki Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ruaha alisema, mifugo hiyo 345 imekamatwa na askari wakiwa doria tarehe 13 na 14 Novemba, ...